Friday, 16 November 2012

BODI YA UTALII TANZANIA (TTB) YAZINDUA MKAKATI WA KUTANGAZA UTALII KIMATAIFA

 
Waziri wa maliasili na Utali Mh. Balozi Khamis Kagasheki akizungumza katika uzinduzi  wa Mkakati wa mpya wa Utangazaji wa Kimataifa wa Utalii wa Tanzania (International Marketing Strategy For Tanzania)mpango uliozinduliwa jioni hii na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam na kujumuisha wadau mbalimbali wanaojihusisha na masuala ya utalii ambapo Waziri Kagasheki ameuzindua rasmi.
(PICHA NAWWW.FULLSHANGWEBLOG,COM)
 
Waziri wa maliasili na Utali Mh. Balozi Khamis Kagasheki akikata utepe katika kitabu kinachoelezea mkakati wa kutangaza utalii wa utalii wa Tanzania kimataifa kutoka kulia ni Bw. Gaudence Temu Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Utalii Tanzania (TCT), Ahmad Khatib Kamishna wa Utalii na kushoto ni Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dkt. Aloyce Nzuki.
Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Balozi Charles Sanga akizungumza katika uzinduzi huo kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dkt. Aloyce Nzuki  akimkaribisha Waziri wa Maliasili na Utalii ili kuzungumza na wageni waalikwa na wadau mbalimbali katika uzinduzi huo.
 
Bw. Gaudence Temu Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Utalii Tanzania (TCT) akielezea mkakati wa kutangaza utalii wa Tanzania kimataifa kwa wadau wa masuala ya utalii waliohudhuria katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Utalii Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Ibrahim Mussa  akikaribishwa katika uzinduzi huo na Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Bi. Devotha Mdachi
Mei.

No comments:

Post a Comment