MKUTANO MKUBWA WA INJIRI IRINGA KUUNGURUMA KATIKA UWANJA WA SAMORA KUVUNJA NGUVU ZA KICHAWI.
Hizi ni siku kumi za miujiza mikubwa ambayo haijapatakutokea katika mkoa wa Iringa kuanzia terehe 23/03/2013 hadi tarehe 03/03/2013, ni katika mkutano mkubwa wa kuvunja na kuharibu nguvu za kichawi ambazo zimekuwa zikiwatesa watu kwa muda mrefu sasa zinakenda kukomeshwa ambapo maandalizi ya mkutano huo yamekamilika na Wahubiri wa kimataifa zaidi ya wanne watakuwepo kuwahudumia watu wa mikoa ya nyanda za juu kusini,ikiwa ni pamoja na mwenyeji wa mkutano Askofu Boaz Sollo, Mtume Ken Gitonga,Bonefasi Indeche pamoja na Dastan Maboya ambapo Askofu Dk.Boaz Sollo alithibitisha kwamba huu ni mkutano ambao haujawahi kufanyika iringa na aliwataka wakazi wa Iringa kushiriki kikamilifu katika mkutano huo ili waweze kuziona Baraka za Mungu katika maisha yao.
Wakati huohuo wakristo nchi wametakiwa kumtumaini mungu na siyo kuogopa nguvu za Kishirikina.
Hayo yamesemwa na askofu wa huduma ya overcomers power centre pamoja na makanisa ya End Time And Havesting Church Dr.Boaz Sollo alipokuwa akifundisha katika ibada zilizofanyika mfululizo wiki iliyopita ikiwa ni moja ya masomo yanayoendelea kufundishwa na mtumishi huyo na kuwataka waumini wa kanisa hilo kutambua namna wanavyo weza kuzishinda nguvu za kichawi ambazo mara nyingi zimeonekana kuwasumbua watu wengi hususani katika mkoa wa Iringa.
Askofu Boaz aliwataka wazazi kutambua umuhim wa kuwalinda watoto wao kwa maombi ili kuwakinga watoto hao na nguvu za kichawi ambazo pia zimeendelea kuwatesa watoto huku wengine wakittumikishwa na kushughulishwa na shughuli za kishirikina lakini pia wengi wameshindwa kuendelelea na masomo kutokana na nguvu za kishirikina,hivyo a matendo ya mitume 13.6 akazungumzia habari za watu kama Bayesu au Elima aliyekuwa akimuhudumia liwali aliyekuja kuokoka na elima kufanya mbinu za kumfanya aache imani kwa hilo pia unaweza kuona jinsi wachawi wanavyofanyakazi ya kurudisha nyuma imani za watu waliomjua mungu kutokana na shuhuda mbalimbali ambazo watu wameweza kushudia na Mungu amejidhihirisha wazi kwamba kuna jambo ambalo mungu ametenda kwa watu wa Iringa kupiia huduma ya mtumishi wa Mungu Askofu Boaz solo,ikiwa bado somo hilo linalo husiana katika mkutano wa Samora Iringa.
No comments:
Post a Comment