Tuesday, 12 February 2013

MWANAMKE ATIMULIWA KWA KUTUHUMIWA NI MCHAWI



Zainabu Zuberi mwenye kitambaa cheusi kichwani akiongozana na askari kanzu pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kuokolewa na askari hao eneo la tukio ili asishambuliwe na wananchi wenye hasira kali wakimtuhumu kuwa ni mchawi


Zainabu Zuberi akituhumiwa kuhusika na ushirikina.


 Mume wa Mtuhumiwa huyo Sulemani Rubea(49) amekataa mke wake kutuhumiwa kwa ushirikina ambapo aliwatupia lawama wanakijiji kwa madai kuwa wanaendekeza udini na kutopenda maendeleo na ndiyo maana hawawataki mtaani hapo.

Moja ya askari akipata maelezo kwa mama aliyepotelewa na mtoto wake katika mazingira ya kutatanisha wiki mbili zilizopita mpaka sasa hajapatikana mtoto huyo





Wananchi hao kwa pamoja waliazimia kumhamisha Mwanamke huyo Mtaani hapo katika mkutano ulihudhuriwa na wakazi zaidi ya 200 ambao walidai kuchoshwa na hali hiyo.


Hii ndiyo nyumba anayoishi anaetuhumiwa kwa uchawi ilolo Mbeya


No comments:

Post a Comment