![]() |
Mama ambaye Mungu amemtendea muujiza siku ya jana kanisani Kawe! |
Tukio hilo lililowaacha watu waliokuwepo kanisani kwa mshangao na kumshukuru Mungu, ni baada ya mama aliyekuwa mjauzito wa miezi saba kuja kanisani pamoja na karatasi za daktari kuwa mwanaye amefariki akiwa ndani ya tumbo.
Akieleza kwa machungu kabla ya kufufuka kwa mwanaye, mama huyo alisema kuwa, huo ulikuwa ujauzito wa pili baada ya mara ya kwanza mtoto wake kutoka kabla ya muda. "Lakini jambo hilo limejirudia tena kwa mtoto huyu wa pili maana baada ya kwenda hospitali niliambiwa kuwa mtoto wangu amekwisha fariki" alisema mama huyo.
Mchungaji Josephat Gwajima alimuombea, na dakika ile ile mama huyo alisikia mtoto akicheza ndani ya tumbo jambo ambalo lilimwacha mama huyo akiwa na furaha... "Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakao onekena tele wakati wa mateso".
No comments:
Post a Comment