Aliyewahi kuwa mtangazaji wa WAPO Radio FM na baadhi ya vituo vingine vya Radio nchini, marehemu Onesmo Ngussa, hatimaye anatarajia kuzikwa leo kwenye makaburi ya Tegeta, jijini Dar es Salaam, na msiba uko maeneo ya Wazo Hill, njia ya kwenda Madale. Kabla ya kwenda Madale, kuna njia inachepuka inayoitwa Umoja Street, na mbele yake kuna mahema.
Ifuatayo ni ratiba ya tukio zima kama ambavyo imeifikia Gospel Kitaa.
SN | MUDA | TUKIO | MHUSIKA |
1 | 10:00 am – 11:30 am | Wageni Kuwasili | MC |
2 | 11:30 am – 12:30 pm | Chakula | Watu wote |
3 | 12:30 pm – 01:30 pm | Ibada (Sifa, kwaya, neno) | MC/ Mchungaji |
4 | 01:30 pm – 02:00 pm | Salamu toka sehemu mbalimbali | MC/ Mchungaji |
5 | 02:00 pm – 03:00 pm | Kuaga Mwili | Watu wote |
6 | 03:00 pm – 03:30 pm | Kuelekea makaburini na ibada ya Maazishi | Mchungaji |
7 | 03:30 pm – 04:00 pm | Kuweka mashada ya maua na kusoma wasifu | MC |
8 | 04:00 pm – 04:30 pm | Shukrani ya familia | Mhusika |
No comments:
Post a Comment