Wednesday, 6 March 2013

PASAKA GOSPEL FESTIVAL CCM KIRUMBA TAREHE 31/3/2013 KUWAKUTANISHA WAKALI WA MUZIKI WA INJILI WANAOTAMBA NCHINI TANZANIA KAMA ENOCK JONAS- ZUNGUKA, NEEMA MWAIPOPO NA WANGINE TISA KUTOKA DAR, MBEYA ARUSHA NA MWANZA.HII SI YA KUKOSAAA.


Meneja wa kampuni mpya ya kurekodi muziki, vipindi na video ya COSU Entertainment Albert G. Sengo (kushoto) akitoa taarifa juu ya uzinduzi utakao kwenda kufanyika Siku ya Pasaka tarehe 31/03/2013 ambapo waimbaji Enock Jonas anayetamba na wimbo wake wa Zunguka pamoja na Neema Mwaipopo maarufu kwa wimbo wa Raha Jipe Mwenyewe na wengine wengi watashuka jijini Mwanza kuupamba uzinduzi huo kulia kwake ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Fabian Fanuel.



UZINDUZI WA KAMPUNI ILIYONUIA KULETA MAPINDUZI KWENYE SOKO LA DIGITALI MWANZA COSU ENTERTAINMENT UTAKAOFANYIKA TAREHE 31/03/2013 SIKU YA PASAKA UWANJA WA CCM KIRUMBA MWANZA .
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ndugu zangu wanahabari.
Ujio wa COSU Intertainment unakuja wakati Tanzania ikishuhudia Media zake zikiingia katika mfumo wa digitali ambao unahitaji kulishwa ipaswavyo ili kuvutia wadau na wafanyabishara kuweza kushawishika kununua muda wa vipindi husika (kuwa wadhamini) jambo ambalo huchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya utoaji huduma kwa media mbalimbali hapa nchini.

Ikumbukwe kuwa awali Taifa letu lilikuwa kwenye mfumo wa Analojia ambao ilikuwa ukiwa na Luninga yako na nishati na antenna yako ya waya basi mawasiliano utayapata utatizama Tv yoyote hata vipindi visivyokuwa na ubora  au usivyokuwa na mpango navyo alimuradi tu umetizama TV, sasa hizo zama zinatoweka taratibu mikoa baada ya mikoa.

Walianza Dar es salaam, Dodoma, Tanga sasa Mwanza nayo imeingia kwenye mfumo wa digitali mwisho wa siku wilayani, vijijini na Taifa kwa ujumla litakuwa digitali.

Kwa hali ya sasa ndani ya mfumo wa digitali ili upate mawasiliano ya televisheni lazima uwe na king’amuzi ambacho unalipia, sasa wamiliki wa ving’amuzi tulivyonavyo (vi 3 sasa) ili kuvutia wateja kwa malengo ya kupata soko kubwa wanalazimika kuweka channel zenye mvuto na zenye ubora ili kukidhi soko la ushindani.
Kupitia ushindani itafika kipindi ndani ya king’amuzi kimoja kutakuwa na chanel  200 hivi za ndani na nje hapa tutashuhudia tukishindanishwa na televisheni za kimataifa, kwa mfumo huu vituo vingi vitakuwa vikishindana kwa kuwa na maudhui nzuri na kuwa na vipindi vya kipekee  ili vipate matangazo na wadhamini wa kutosha.

Ni suala lililo wazi kuwa wenye matangazo yao hukimbilia vituo vinavyotizamwa.

Media kwa sasa ziko kwenye mahitaji ya kiushindani, hivyo zina mahitaji na mahitaji, kwa mtindo huu basi COSU Entertainment tumeona kuwa kuna mwanya hapo, nasi ni vijana wakongwe katika tasnia ya media tuko kwaajili ya kuuziba mwanya huo, na hizi ndizo juhudi sasa za kuitikia wito wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA kuzifanyia kazi zile ajira ambazo tumeelekezwa zipo nasi kushuhudia kweli zipo.

COSU Entertainmen tuliojikita zaidi katika uandaaji na utayarishaji kuanzia vipindi, Audio music, Video za muziki pamoja na kujenga jukwaa la vipaji mbalimbali nchini Tanzania tumeliona soko hilo la ajira na sasa tunataka kuudhihirishia umma wa Watanzania kuwa mapinduzi yatafanyika kupitia sisi.

Hatujaishaia hapo pia tumeliona soko jingine la ajira lililopo vijijini na wilayani hapa tunazungumzia Muziki wa Asili, huu ni muziki ambao kwa sasa vionjo vyake vinakuja kwa kasi na kuboresha muziki wa kisasa na muziki huo wa asili ukionyesha kuwa na dira ya maisha marefu sokoni.

Tizama marafiki zetu Afrika Magharibi, Afrika ya kati, Afrika ya kusini wote hao vionjo vya muziki asili vimechangia kuubeba sana muziki wao kutamba katika soko la kimataifa na sasa ndiyo wameiteka dunia.
Mifano iko mingi – akina Werason, Koffi  Olomide, Fally Ipupa, J. Martins na wengine wengi wote hawa style zote mpya wanazokuja nazo nyingi zinatoka vijijini, ambako hufanya mashindano ya vipaji mbalimbali iwe waimbaji, wapigaji muziki hadi wachezaji na kuubebea muziki huo kwenye soko hatimaye makubwa mapinduzi tunayashuhudia.

Sasa kwa hili tukirejea nchini na kuanzia hapa Kanda ya ziwa, Kanda inayosifika sana kwa vipaji vya nyimbo asili tena za kuchezeka, anzia Kagera kwa akina Saida Karoli, Maua, Papaa Kishaju wote muziki wao unadumu, Ingia Shinyanga kuna ngoma asili pale kama Bolaboka, Wigashe, Bogobogobo, rudi Mwanza na wilaya zake nenda Ukerewe na Kadogoli, Dungu, ngoma nyingi za kuchezeka tena za kusisimua na hata tumeshuhudia mara nyingine zikitumika kwenye  maharusi na dhifa mbalimbali na kadhalika.

Hivyo basi nina uhakika tukitumia vyema muziki huu mengi yatafanyika.

Katika project tutakazozifanya kuna watu wakajkuja kwetu kurekodi kwa fedha na kuna watu tutawasaka nao warekodi kwa gharama zetu hawa ote tutashirikiana nao kutengeneza matirio zenye maudhui ya kuuzika, zenye Ushawishi.

Ndugu zangu waandishi wa habari huduma zetu ingawa zimeanza kufanya kazi kwa kurekodi baadhi ya vipindi kwaajili ya vituo vya televisheni mbalimbali, pamoja na kurekodi video za kwaya na bendi mbalimbali kwa sasa, uzinduzi rasmi tutaufanya mnamo tarehe 31/03/2013 katika sherehe ya sikukuu ya Pasaka uwanja wa CCM Kirumba ambapo tutafanya tamasha la Muziki wa Injili tulilolipa jina la PASAKA GOSPEL FESTIVAL ambapo wakazi wa Mwanza watashuhudia tamasha lililoandaliwa kwa ubunifu wa hali ya juu likishirikisha waimbaji wakubwa kama Enock Jonas (ZUNGUKA), na Neema Mwaipopo (RAHA JIPE MWENYEWE).

Wengine ni Nesta Sanga (JIANDAENI), Danni Safari, John Shahban, Jeska Julius, Isaya Msangi (SHETANI IMEKULA KWAKO), Danny Sanga kutoka Iringa, Tumaini Mbembela  kutoka Mbeya na mkoa wa Arusha utawakilishwa na Neema Munisi.

Kwaya za mkoa wa Mwanza ni nyingi za kutosha Anglican Vijana kwaya, EAGT City Centre kiufupi kwa zote zitaweka kambi kwenye shughuli yetu ya Pasaka.

Jumatatu ya pasaka tutakuwa Geita uwanja wa CCM Katoro
Kiingilio kwa maeneo yote kitakuwa ni shilingi. 2000/= tu
Hivyo tunawakaribisha wote kwenye uzinduzi huo.

Nanyi ndugu zangu wanahabari twawaomba mtusambazie habari hizi kwani hili linatoka kwa watu wenu na msishangae waandishi nanyi kupitia vipaji vyenu mkapata fursa katika soko la ajira la COSU Entertainment, tukawa tukiwakodisha mara kadhaa kutokana na either kuzidiwa na mahitaji hivyo tunawasihi msisite kufungua milango ya ushirikiano ili tujenge Tanzania yetu.

Zidumu fikra za Maendeleo!
Aksanteni kwa kutusikiliza.



No comments:

Post a Comment