Friday, 29 March 2013

UMOJA NI NGUVU HASA KATIKA WAKATI HUU AMBAO OVERCOMERS POWER CENTRE WAKIONYESHA JITIHADA ZAO ZA KUJENGA NYUMBA YA BWANA ENEO LA ZIZILANG'OMBE MANISPAA YA IRINGA NA HUU SIYO WAKATI WA KUKAA KWENYE NYUMBA ZENYE MAPAMBO HEKARU LA BWANA LINAHARIBIKA.

Kauli hii inajidhihirisha wazi katika kipindi hiki kigumu ambacho waumini wa kanisa la Overcomers Power Centre (OPC) wakikabiliwa na ujenzi wa nyumba ya Mungu kwa kutumia nguvu zao pamoja na muda wao kuhakikisha wanapata mahali pa kuabudia,Mchakato wa ujenzi wa kanisa hilo ulianza kwa kutafuta eneo la kujenga Hekaru hilo kwa kuchangia kiasi cha fedha ambazo waumini hao waliwiwa kutoa ili kusaidia ununuzi wa kiwanja cha ujenzi wa kanisa hilo haikuwa kazi rahisi kufikia mahali walipo fikia leo hata ukiangalia katika picha zilizowekwa hapo chini na hiyo ndiyo uhalisia wenyewe kwamba waumini hao wamedhamilia kumjengea Mungu Hekaru,

Miongoni mwa kauli nzuri zilizotolewa na Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo alisema miongoni mwa malengo ya ujenzi wa kanisa hilo ni kuhakikisha watu wa mkoa wa Iringa na nchi nzima wanabadilishwa mitazamo ya kidunia na kuachana na kumgeukia mungu lakini pia ni kuwa kanisa litakalohakikisha watu wa mkoa wa Iringa wana pata mafundisho ili kujikwamua kiuchumi kiroho na pi ni kutengeneza mahusiano mazuri ya kiroho na waumini wa madhebu mengine hasa kupitia kituo cha Redio ya Kanisa hilo iitwayo OVERCOMERS FM ambayo ni maarufu katika mikoa ya nyanda za juu kusini inayopatikana katika masafa ya 98.6 Iringa.

Huduma inayotolewa na kanisa la Overcomers Power Centre imefanyika Baraka kubwa kwa wakazi wa mikoa hiyo ya nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla na hii inajidhihirisha kutokana na jinsi watu wanavyofunguliwa pia wanavyo barikiwa na kufanikiwa katika maisha yao.

Harambee ya uchangiaji fedha kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo.

Ili kuthamini michango inayotolewa na viongozi mbalimbali hapa nchini katika kuhakikisha kazi ya mungu inasonga mbele Kanisa la Overcomers Power Centre Iringa chini ya mtumishi wa Mungu Askofu Dk Boaz Sollo limeandaa tuzo maalum nayaheshima kwaajili ya kumtunuku Waziri mkuu aliyejihuzuru Mh Edwadi Lowasa ambaye ndiye atakayekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo inayotarajiwa kufanyika tarehe 21/04/2013 hapo mkoani Iringa kwaajili ya ujenzi huo.

Akizungumzia kuhusu tuzo hiyo Askofu wa kanisa hilo Dk Boaz Sollo amesema kwa kutambua mchango wa kiongozi huyo wa nchi katika kuyasaidia makanisa pamoja na shughuli za kijamii wameona ni vyema kumtunuku tuzo ya Heshima ili kumtia moyo kwa kazi anayo ifanya kwa jamii pamoja na changamoto nyingi anazokutana nazo wakati wa kujitolea na kusaidia suala la maendeleo katika jamii hasa wale wanao mpinga katika hilo ili kumkatisha tamaa hivyo Askofu Boaz Sollo pamoja na waumini wa kanisa hilo wataendelea kumuombea ili afanikiwe zaidi pamoja na kushinda vikwazo vinavyomkabili kiongozi huyo.

"tunatambua mchango wake kwa jamii na amesaidia makanisa mengi wau wengi pamoja na vikundi vingi  kwakweli ni mtu wa watu kwa kuliona hilo tumeona siku hiyo ya Harambee tutamtunuku Tuzo ya heshima ili kumtia moyo na asikate tamaa kuendelea kuwasaidia watu mbalimbali pale wanapomuhitaji"

"tumeona mchango wake na tumeguswa na hilo sisi tutendelea kumuombe kwa Mungu ili afanikiwe katika yale anayoyafanya hata kama kuna watu wanaompinga hii inatokana kwamba siku zote tunaamini shetani hapendi maendeleo ya mtu wa Mungu"alisema askofu.

Kwa upande wa wananchi wa mkoa wa Iringa walipongeza kanisa hilo kwa kukumbuka kumpa tuzo kiongozi hiyo ambaye tangu ajihuzuru uongozi wake hakuwahi kufika Iringa na ameendelea kujitolea katika shughuli za jamii bila kubagua rangi au kabila la watu anaoweza kuwasaidia,hivyo wanamsubiri kwa hamu kubwa ili kumuunga mkono kwa shughuli atakayo ifanya ya kuongoza uchangiaji wa ujenzi wa nyumba ya bwana 

Haya ni majengo ya Ofisi pamoja na kituo cha redio ya Overcomers fm

Jengo hili la Ofisi za kanisa hilo pamoja na Kituo cha Redio
Mafundi wakiendelea na kazi ya Ujenzi wa ofisi za kanisa
Upende wa nyuma wa Ofisi
Upande wa mbele wa jengo la Ofisi na huo msingi mbele yake ndimo utakamopita ukuta wa kanisa lenyewe
Nguvu kazi ya waumini wa kanisa hilo la Overcomers Power Centre zikionekana hapo

Wednesday, 20 March 2013

WAKALI WA MUZIKI WA INJILI KUTOKA MWANZA BAPTIST CHIPUKIZI KWAYA WATIBITHISHA KUSHIRIKI PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2013 CCM KIRUMBA MWANZAA

Baptist Chipikizi Kwaya

Moja kati ya kwaya zinazofanya vizuri katika anga la muziki wa injili Mwanza na Kanda ya Ziwa Baptist Chipukizi Choir kutoka Usagara Mwanza wametibithisha kushiriki katika Pasaka Gospel Festival 2013 katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Wakiongea na mtandao huu wamesema wao wamejipanga vizuri kuja kutimiza kusudi la kusherehekea pasaka kwa kishindo kisichokuwa cha kawaida kama jinsi watu wanavyowajua.
Pasaka Gospel Festival 2013 inayoandaliwa na Cosu Entertainment itafanyika jumapili 31/3/2013 katika uwanja wa CCM Kirumba na 1/4/2013 katika uwanja wa CCM Katoro Geita. 
Huku wakazi wa mikoa wa Mwanza, Geita, Mara, Kagera, Shinyanga, Simiyu, Kigoma na Tabora wakiwa na ari ya kushuhudia Pasaka Gospel Festival kwa uhalisia wake.

Pasaka Gospel Festival 2013 litaongozwa na Mkali wa Muziki wa Injili kutoka Dar es salaam Enock Jonas Zunguka Zunguka, na Gwiji wa muziki afrika masahariki Neema Mwaipopo na wasanii wengine kumi kutoka Dar, Mbeya, Arusha, Tabora, na Iringa.

Kwaya zaidi ya kumi na tano zitapiga kambi kwa ajili ya kutumbuiza katika tamasha hilo kwa kingilio cha 2000/= kwa wote.

Friday, 15 March 2013

Watu wanne wafikishwa mahakamani wakituhumiwa kumuua kwa maksudi John Mwankenja aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiwira(CCM) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe..



 Marehemu John Mwankenja aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiwira(CCM) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe..



Watu wanne wamefikishwa katika mahakama kuu kanda ya Mbeya wakituhumiwa  kumuua kwa maksudi John Mwankenja aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiwira(CCM) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe..
Mwendesha mashtaka wa Serikali Basilius Namkambe aliaambia Mahakama hiyo Mbele ya Jaji Samweli Karua kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Mei 15,2011 katika Kijiji cha Mpandapanda kata ya Kiwira Wilayani Rungwe kinyume na kifungu cha 196(16) kilichofanyiwa marekebisho Mwaka 2002.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Hakimu Mwakalinga ambaye ndiye mtuhumiwa namba moja katika kesi hiyo akiwa na Daudi Mwasipesya,Obote Mwanyimbili na Kelvin Maurus Myovela ambao wanatuhumiwa kumuua John Mwankenja aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiwira(CCM) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe.
Awali baada ya kupandishwa kizimbani watuhumiwa kujibu kesi inayowakabili yenye namba 31/2012 walimkataa Wakili aliyejulikana kwa jina moja laMwakabubu aliyekuwa ameteuliwa kwa ajili ya kuwatetea kwa madai kuwa hawana imani naye kutokana na mwenendo wa kesi alizosimamia.
“Mtukufu Jaji kabla ya kesi yetu haijaanza kusikilizwa tunaomba kubadilishiwa Wakili kwa sababu huyu Mwakabubu hana uwezo na tumeona kesi ndogo tu anababaika na kesi yetu ni kubwa tunaona wazi kabisa kuwa hataweza kututetea” alisema Mwakalinga Mshitakiwa namba moja.
Kufuatia ombi hilo Jaji Karua alikubaliana nao ambapo alimteua Wakili mwingine ambaye ni Sambwee Shitambala ambaye walimkubali kabla hajawaongezea wakili mwingine ili asaidiane na Shitambala ambapo alimtaja Wakili Zakia Selemani.
Akisoma mashtaka yao Mwendesha mashtaka wa Serikali Basilius Namkambe  aliiambia mahakama hiyo kuwa mnamo tarehe 19, Mei 2011 majira ya jioni marehemu akiwa anatokea Mbeya mjini akirudinyumbani kwake Kiwira Wilayani Rungwe alifika Nyumbani akiwa na gari lenye namba za usajili T 127ACZ Nissan (Double cabin).
Namkambe aliongeza kuwa baada ya kufika nyumbani kwake alipiga honi ya gari kwa ajili ya kuomba kufunguliwa geti la mlango ambapo baada ya kusikia honi hiyo alitoka Mjomba wake ambaye baada ya kumfungulia aliambiwa ashushe Kuku aliyokuwa amewabeba nyuma ya gari yake.
Alisema kabla ya mjomba wa Marehemu hajaanza kushusha kuku kwenye gari alitokea mshitakiwa namba moja akiwa na siraha ambapo alimwamuru asifanye lolote ndipo akaanza kufyatua risasi akimwelekezea marehemu kisha kumuuana kutoweka kusiko julikana.
Akijibu tuhuma hizo Wakili wa Utetezi Shitambala na Zakia walikana washtakiwa hao kuhusika na matukio hayo pamoja na baadhi ya vielelezo vilivyotolewa na upande wa mashtaka kuthibitisha kuhusika kwa wateja wao.
Walisema mtuhumiwa wa kwanza hakuwepo Wilayani Rungwe siku ya tukio ambapo walisema atakuwa na mashahidi ambao watathibitisha kwamba hakuhusika ambao waliwataja kuwa ni pamoja na yeye mwenyewe, Askari Magereza wawili wa gereza la Tukuyu Wilayani Rungwe waliotajwa kwa jina moja moja la Hereda na Green.
Wengine ni Padeso Mwakipesile, Aneth Siandene Kalinga na Jumanne Mwakisole huku washtakiwa namba mbili, tatu na nne ambao hawatakuwa na mashahidi ambapo watasimama wao wenyewe kujitetea.
Namkambe aliiambai mahakama hiyo kuwa upande wa mashtaka utakuwa na mashahidi zaidi ya 15 ambao aliwataja kuwa ni pamoja na Sofia Fungameza, Weston Gilbert,Magdalena Mgawe, Musa Jackson, Issa Mwaipopo, Teresia Ludovick na Williamu Mtanga.
Wengine ni askari Polisi Mwenye namba D2385 Sajent Michael wa Tukuyu, Inspekta Isaya Bwile wa Tukuyu, David Paul kutoka makao makuu ya Polisi Dar Es Salaam, Twaha kutoka kitengo cha Upelelezi makao makuu ya Polisi Dar Es Salaam, Haruna kutoka Polisi Tukuyu na WP3433 Agnes wa polisi Tukuyu.
Namkambe aliwataja mashahidi wengine katika kesi hiyo kuwa ni pamoja na aliyekuwa Mkuu wa upelezi (RCO) Mkoa wa Mbeya aliyehamishiwa makao makuu SSP Anacletus Malindisa, John Mayunga na Dk. D Z Matata kutoka ofisi ya Mkemia mkuu wa Serikali.
Jaji Karua aliahirisha kesi hiyo hadi hapo itakapopangwa tena kwa ajili ya kuendelea na kuwasilikiza mashahidi kutoka upande wa mashtaka baada ya kuambia mahakama kuwa upelelezi umekamilika na mashahidi wote wako tayari.

MITUME WALIOPO NCHINI KWA MASLAHI YAO BINAFSI HAO HAWAJATUMWA NA MUNGU, NI MATAPELI NA HULIPELEKA TAIFA KUPOTEZA AMANI

MKURUGENZI JEREMIA MWAKANYILENGE 



WAANDISHI WA HABARI WAKIWA OFISI YA JEM MINISTRY WAKIONGEA NA MKURUGENZI JEREMIA MWAKANYILENGE

-->
KWAKUA MITUME WA KWELI YEYE NI MUHUDUMU WA JAMII NA MUNGU HUYAFANYA MAMBO MAGUMU KUWA MEPESI

Hayo yasememwa na mtume JEREMIA MWAKANYILENGE wa huduma ya Jem ministry ya jijini mbeya alipokuwa akiitambulisha huduma hiyo kwa waandishi wa habari ofisini kwake.

Mwakanyilenge amewataka waumini kuwa makini sana na huduma hizi zilizoshamili kuibuka kila siku kutokana na kuwepo na baadhi ya watumishi matapeli wanaotumia jina la kristo kujinufaisha wenyewe binafsi

“Ukiona mtume huduma yake inaleta uchochezi katika taifa hili ujue huyo si wa mungu atakuwa amejituma mwenyewe na ni tapeli, kwani aliyetumwa na mungu kweli huyafanya yaliyo magumu kwa watu kuwa mepesi” amesema mwakanyilenge.

Katika kikao hicho pia alipata nafasi ya kuitambulisha rasmi hudu yake ya JEM MINISTRY kua si kanisa jipya bali ni tasisi ya kuihudumia jamii kwa kuwapatia ajira katika idara zake za biashara kama vile JP PRODUCTION studio inayofanya kazi za kurekodi audio cd pamoja na video, lakini pia imeanzisha mfuko wa kustaafu wachungaji.

JP PRODUCTION imetoa ajira kwa wachungaji na vijana mbalimbali wenye kipaji cha uimbaji kwa kujikimu na maisha yao kama wengine, Lakini pia imekuwa ikisambaza kazi za waimbaji kwa kuwapa faida kubwa kuliko wasamabazaji wengine.

Kwa hivi sasa JEM MINISTY pamoja na JP PRODUCTION imeto kazi mpya ambayo ipo sokoni yenye nyimbo nane zilizoimbwa live na mtumishi wa mungu JEREMIA MWAKANYILENGE kwa kushirikiana na mwaimbaji wa kimataifa EFRAIM SEKELETI toka nchini zambia.

Thursday, 14 March 2013

ENOCK JONAS ZUNGUKA ZUNGUKA NDANI YA JIJI LA MWANZA NA GEITA PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2013

Mwimbaji anayetisha sana katika medani ya muziki wa injili ENOCK JONAS ambe anatamba na wimbo wake wa Zunguka Zunguka, amesema Pasaka ya Mwaka huu atakula na wakazi wa jiji la Mwanza na Geita na hii ni kutokana na mapenzi aliyonayo kwao.

Enock Jonas amesema anakuja kutambulisha albaumu yake mpya iitwayo NIPE MDUNDO albamu ambayo ina kila sababu ya kupewa sapoti na wadau wote wa muziki wa Injili kanda ya ziwa.

Pasaka Gospel Festival 2013 litafanyika tarehe jumapili tarehe 31/3/2013 katika uwanja wa CCM Kirumba na tr 1/4/2013 katika uwanja wa CCM Katoro Geita kwa kiingilio 2000/= kwa kila mtu.

Wednesday, 13 March 2013

PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2013 CCM KIRUMBA MWANZA PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2013 CCM KIRUMBA MWANZA, KUTANA NA ISAYA MSANGI KATIKA WIMBO WAKE SHETANI IMEKULA KWAKO. USIKOSE SIKU HIYO. Isaya Msangi - Shetani Imekula Kwako


Mwimbaji wa anayetisha katika Muziki wa Injili kutoka Dar es salaam Isaya Msangi anayetamba na wimbo wake wa shetani imekula kwako amesema anakuja Mwanza kwenye Pasaka Gospel Festival kuwapa Raha wakazi wote wa Jiji la Mwanza na Mkoa wa Geita.

Msangi ambaye amezindua albamu yake Jumapili iliyopita Jijini Dar es salaam amesema kuwa kutokana na kukubalika sana mikoa hasa Mwanza amewaomba watu wote wajitokeze kujionea jinsi Mungu anavyomtumia katika nyimbo za Injili.

 Mbali na Isaya Msangi, katika Tamasha Hilo La Pasaka Gospel Festival 2013 wapo waimbaji kama Enock Jonas,Neema Mwaipopo, Nesta Sanga, Daniel Safari, Jessica Julius, John Shaban wote kutoka Dar es salam, Kutoka Mbeya yupo Tumaini Mbembela, Kutoka Iringa Dan Sanga na Arusha yupo Neema Munis. Pia wapo waimbaji na kwaya kali kutoka Mkoa wa Mwanza na Geita katika kusherekea sikukuu ya Pasaka.

Pasaka Gospel Festival 2013 litafanyika tarehe 31/3/2013 katika uwanja wa ccm kirumba na tarehe 1/4/2013 katika uwanja wa ccm katoro Geita kwa kiingilio cha 2000/= kwa kila mtu.

Karibuni sana watanzania wote wa dini, rangi, rika zote.

Tuesday, 12 March 2013

AIC BWIRU CHOIR WANA WA DIGITALI WAZINDUA KWA KISHINDO ALBAMU YAO YA CHOMOKA NA AMSHA AMSHA ZA PASAKA PANDE ZA BWIRU..


Monday, 11 March 2013

NESTA SANGA: MWIMBAJI NGULI KUTOKA DAR ES SALAAM NDANI YA TAMASHA LA PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2013 CCM KIRUMBA TR 31/3/2013 NA TR 1/4/2013 CCM KATORO GEITA. JIONEE MWENYEWE ILI MACHO YAKO YAFAIDI KUELEKEA PASAKA MWAKA HUU MWANZA NA GEITA.



NESTA SANGA.




Mwimbaji anayetisha katika medani ya muziki wa injili Tanzania kutoka Dar es Salaam Nesta Sanga amekuwa mwimbaji mwingine kuthibitisha kuimba katika Tamasha la Pasaka Gospel Festival 2013 litakalofanyika katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 31/3/2013 na tarehe 1/4/2013 katika uwanja wa CCM Katoro Geita.

Nesta ambaye kwa sasa anatamba na albamu yake mpya iitwayo TWENDENI ameweka wazi alipoongea na waandishi wa habari kuhusu maandalizi yake kuelekea tamasha hilo na kusema kuwa ashukuriwe Mungu ambae amempa nafasi katika tamasha hili la Pasaka Gospel Festival 2013.

Amesema kuwa yeye kama Nesta amejiandaa vya kutosha kuja kuwapa wakaazi wa Mkoa wa Mwanza na Mkoa wa Geita vitu vya ukweli ambavyo hawatakaa wasahau kamwe.

Pia amewaomba watu wote wa dini zote na wasiokuwa na dini kujitokeza kuja kujipa raha kaitka kusherehekea pasaka mwaka huu katika uwanja wa CCM Kirumba na CCM Katoro Geita.

'' Nawaomba watu kuja siku hiyo kuona vipawa na nyimbo ambazo Mungu ametupa ili tuweze kubarikiwa kwa pamoja, na vilevile kumshukuru Mungu kwa ajili ya kumbukumbu ya kufa na kufufuka kwa Yesu Mwokozi'' alisema Nesta.

Tamasha la Pasaka Gopsel Festival 2013 litawakutanisha waimbaji kutoka Dar es Salaam, Mbeya, Iringa, Arusha, Tabora, Mwanza na Geita. Waimbaji kutoka Dar es Salaam ni Enock Jonas[ Zunguka Zunguka] Neema Mwaipopo[ Raha Jipe Mwenyewe] Nesta Sanga[ Jiandaeni] Isaya Msangi[ Shetani Imekula kwako] Daniel Safari, John Shaban, Jessica Julius, Tumaini Mbembela kutoka Mbeya, Dan Sanga kutoka Iringa, Vedasto kutoka Tabora, Neema Munis kutoka Arusha na kwaya na bendi mbalimbali kutoka Mwanza na Geita.

Tamasha hilo litakuwa kwa gharama ya shilingi 2000/= kwa kila mtu katika maeneo yote ya Mwanza na Geita.

TAMASHA LA PASAKA GOSPEL FESTIVAL 2013 MWANZA HILO LAKARIBIA, NA HIZI NI AMSHA AMSHA ZAKE KATIKA UWANJA WA SHULE YA MSINGI BUHONGWA. TAZAMA MWENYEWE.

 Watu kutoka maeneo ya Buhongwa na maeneo ya karibu wakitazama yale mazuri yaliyokuwa yakiendelea katika viwanja vya Shule ya Buhongwa katika amsha amsha za Pasaka Gospel Festival 2013.
                                  Imani Baptist Kwaya Sahwa wakitumbuiza stejini.
                   Watu wakitazama kwa umakini kwenye tamasha la amsha amsha ya Pasaka.
 Meneja wa Cosu Entertainment ambae pia Mratibu wa tamasha la Pasaka Gospel Festival 2013 ambalo kilele chake kitafanyika katika uwanja wa CCM Kirumba tr 31/3/2013 na tr 1/4/2013 katika uwanja wa CCM Katoro Geita kwa kiingilio cha 2000/= kwa kila mtu.
                                         Tazama mwenyewe shughuli ilivyokuwa.
                                  Hapa wanambomoa shetani katika staili ya bomoa bomoa.
                                                 Uwepo wa Mungu ukishuka.
                                                    Kila mmoja anatazama kivyake.
                                                           Kitu red in kala uwanjani.
                                                    Tazama mambo zenyewe.
                                                    Unahisi ni staili ipi hii?
 Watu wakiangalia yale mazuri kutoka kwa watoto wa Mungu katika tamasha la amsha amsha ya Pasaka 2013 ambalo litawakutanisha waimbaji wakubwa kama vile Enock Jonas[ Zunguka] Neema Mwaipopo[ Raha Jipe Mwenyewe] na wengine wengi kutoka Dar, Mbeya, Arusha, Iringa na Tabora.

                                     Baptist Nyang'homango wakiwa steji ni kama hiviiiiii.

Hata watoto wadogo nao walitazama kile kizuri kutoka wa kwaya mbalimbali nzuri katika tamasha la amsha amsha za pasaka.